Kiswahili 5
Chagua muundo wa faili unaopendelea na upakue salama kwenye simu yako, kompyuta au kompyuta kibao kusoma na kusikiliza mkusanyiko wa mahubiri wakati wowote na mahali popote. Vitabu vyote pepe na vitabu vya sauti ni bure kabisa.
Maneno katika kitabu hiki yatatosheleza kiu ya moyo wako. Wakristo wa nyakati hizi wanaendelea kuishi pasipo kufahamu suluhisho halisi la dhambi za kila siku watendazo kila kukicha.
Je, unafahamu juu ya haki ya God? Nadhani utajiuliza mwenyewe juu ya swali hili na hatimaye kuamini juu ya haki ya God ambayo imedhihirishwa kupitia kitabu hiki.
Haki ya God imekuwa ikiandamana na Injili ya maji na Roho. Hata hivyo kama ilivyo hazina yenye thamani imekuwa ikifichwa mbali na macho ya wafuasi wa washika dini wengi kwa miongo kadhaa. Namatokeo yake watu wengi wamekuwa wakitegemea na kujigamba juu ya haki zao binafsi badala ya ile haki ya God. Kwa hiyo kanuni za Kikristo zisizo na maana zimetawala imani katika mioyo ya waumini wengi huku wakidhani kwamba ndizo zenye haki ya God.
Kanuni za kuchaguliwa toka asili, kuhesabiwa haki na utakaso wa awamu kwa viwango, ni mojawapo ya kanuni kuu za mafundisho ya wakristo ambayo yameleta tafrani za kimawazo na utupu ndani ya nafsi za waumini.
Lakini sasa, wakristo wengi imewapasa kurudi na kuelewa upya juu ya God, kujifunza juu ya haki yake na hatimaye kuendelea na imani iliyo na uhakika.
"Bwana wetu aliye haki ya God" atakupatia nafsi yako uelewa mkuu na kukuongoza katika amani. Mwandishi anapenda uhodhi baraka ya kuifahamu haki ya God.
Baraka ya God iwe nanyi.
Ingawa janga la Covid-19 limeisha, bado kuna ugumu wa kutuma au kupokea vitabu vyetu vilivyochapishwa kwa Posta kwa sababu ya hali mbalimbali ngumu za kimataifa. Wakati hali ya kimataifa itakapoboreka na utumaji barua kuwa wa kawaida, tutaanza tena kutuma vitabu vilivyochapishwa.