• 所有新生命宣教會 The New Life Mission 網站上的電子書和有聲書均可免費下載
  • 探索以多種語言提供的全球性講道
  • 查看我們已翻譯成27種語言的網站
  • 第1、2卷新修訂版已全新推出
Search

關於基督教信仰的常見問題解答

話題 1:重生於水和聖靈

1-16. Upi ni mshahara wa dhambi?

Mshahara wa dhambi ni mauti. Haijalishi ni dhambi ipi au ya namna gani, kila dhambi itahukumiwa mbele ya Mungu, na hukumu ya kila dhambi ni kifo. Ili tuweze kupata upatanisho wa dhambi, watu wa Israeli iliwapasa kutoa kondoo asiye na doa mbele ya Mungu. Lakini aina hii ya sadaka haikuweza kwa namna Fulani kutakasa dhambi zote kwa wakati wote, “maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi” (Waebrania 10:4).
Kwa hiyo, Mungu alitayarisha sadaka ya Kondoo kukomboa watu toka dhambini. Kila mnyama wa sadaka alipaswa kuwekewa mikono kuweza kubeba dhambi zote na kufa badala yao.
Katika Agano Jipya, Yesu alichukua dhambi zote kwa kupitia ubatizo wake katika mto Yordani akiwa ni Mwanakondoo wa Mungu na kufa kwa ajili yetu. “Mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu” (Warumi 6:23).
Mshahara wa dhambi ni mauti, lakini Yesu alionyesha upendo wake kwa kufa badala yetu na kutuletea zawadi ya uzima wa milele kwa sisi wale tulio wenye dhambi ulimwenguni.
The New Life Mission

參加我們的調查

您是如何得知我們的?